Karibu

Karibu kwenye Tovuti ya CIL. Ligi ya Kutengwa inatoa huduma kwa Kaka na Dada za Christadelphian, na familia zao, ambao wametengwa na eklesia yao. Huduma hutolewa kwa ombi la eklesia yako, hata hivyo unaweza kufikia nyenzo zetu zote kwenye tovuti hii, iwe umejitenga au la.

Huduma zetu ni pamoja na:

  • Mawaidha ya mara kwa mara, Mafunzo ya Biblia na Mihadhara
  • Shule ya Jumapili na Shughuli za Vijana
  • Majarida ya Braille, vitabu na mawasiliano
  • Maktaba ya Rekodi za sauti na video
  • jukwaa la mikutano ya mtandaoni (CIL Meet)

Tafadhali wasiliana nasi ili kujua zaidi.

Ili kupata nyenzo zetu kwenye wavuti yetu, tafadhali jiandikishe na uingie . Unaweza kuona hakikisho hapa chini!

Sasisho za hivi karibuni

Jumapili

Jumapili, 10 Agosti 2025

Masomo: 1 Wafalme 4-5; Yeremia 31; Marko 5 

1 Wafalme 5:

Namna tunavyoshughulika na wengine wakati wote kunakuwa na matokeo ya kudumu. Kwenye 1 Wafalme 5:12 Sulemani aliweza kuandaa vifaa vya ujenzi wa hekalu kwa kumshirikisha Hiramu, kwa sababu ya hekima aliyoipata kwa Mungu. Daudi alikuwa ameweka kielelezo kizuri kwa Hiramu, na vizazi vilivyofuata vikanufaika. 

Yeremia 31:

Kufurahi katika Tumaini

Jumapili, 03 Agosti 2025

Masomo: 2 Samweli 20-21; Yeremia 24; Warumi 12 

Kuna vipengere vingi vinavyotofautiana kwenye ushirika wetu. Tulipobatiziwa Yesu, ushirika wetu ulianzia hapo kuwa na Baba na Mwanawe. Hili liliyabadili maisha yetu, na hasa kwa kuangalia vile tunavyohusiana na kufanya mambo kwa kuzingatiana. 

Kwa kuwa tumekuwa wafuasi wa Yesu na tuna ushirika na ndugu zetu wengine, tunaandikiana meseji na kupigiana simu, na kukutana pale inapowezekana. 

Maji ya Uzima

Jumapili, 27 Julai 2025

2 Samweli 13; Yeremia 17; Mathayo 28 

Unabii wa Yeremia ni kitabu kirefu kwenye Biblia, na unayapitia maisha ya Yeremia ya zaidi ya miaka 40. Alitumikia chini ya wafalme watano, mmojawapo akiwa Yosia; mfalme mwema. 

Pamoja na urefu wa kitabu chake, ujumbe wa Yeremia ni mmoja tu, na hakurudi nyuma; alikuwa mwaminifu mpaka mwisho. Watu walikuwa wakianguka; karibu wote hawakuwa wakimfuata Mungu. 

Jukumu la Yeremia lilikuwa kuwaonya kuwa wangehukumiwa, na aliwasihi wakati wote wamgeukie Mungu. Kwa bahati mbaya ujumbe wake haukusikilizwa; watu hawakumwitikia, na hukumu ilikuja kwa mkono wa Nebukadreza. 

“Wa Kwanza Atakuwa Wa Mwisho”

Jumapili, 20 Julai 2025

2 Samweli 4-5;  Yeremia 10; Mathayo 21 

Tunasoma kwenye Maandiko kuwa Bwana Yesu aliwafundisha watu, akiwa “kama mtu mwenye amri” (Mathayo 7:29). Hakufundisha kama Waandishi; watu wa mamlaka; wasomi. Alikuwa makini; mwenye kujua na kutambua ujumbe aliotaka kuutoa. 

Sidhani kama kulikuwa na haja ya yeye kupiga kelele; alifundisha kwa utulivu. Ni kama nabii Isaya alivyosema akimtabiria Masihi, akisema: “Hatalia, wala hatapaza sauti yake, wala kuifanya isikiwe katika njia kuu” (Isaya 42:2). 

“Watauwa wa Bwana Hulindwa Milele”

Jumapili, 13 Julai 2025

1 Samweli 26-27; Yeremia 3; Mathayo 14 

Kwenye Yohana 17 tunayo maombi yale ya kusisimua kati ya Bwana wetu Yesu na Baba yake, Mungu. Yanaonesha utambuzi wake kuwa, wanafunzi wake ni Baba yake aliyempa (Ms. 2,6,7 n.k.) 

Wazo hili la ‘kupewa’ linatokana na kilichopo kwenye Sheria ya Musa, na mahusiano kati ya Mungu, Kuhani Mkuu na Walawi. Kwa mfano, katika Hesabu 8:14-22 tunasoma kuwa Walawi walitengwa kwa ajili ya Mungu, na hivyo wakawa ‘mali’ ya Mungu. Kwa kuwatenga, Mungu aliwatoa kwa Kuhani Mkuu kwa ajili ya huduma yake. 

Upendo, Uaminifu na Njia ya Haki

Jumapili, 06 Julai 2025

 1 Samweli 18; Isaya 62; Mathayo 7 

Leo nasaha zetu tunazipata kutoka kwenye milango yote mitatu ya kwenye Maandiko yetu: 1 Samweli 18, Isaya 62 na Mathayo 7. Ingawa yote inaongelea mambo yanayotofautiana na nyakati ni tofauti, vifungu hivi vinatuletea mafundisho yanayotugusa sote, yakihusiana na upendo, uaminifu na kuifuatia njia ya haki. 

Tunavyoitafakari milango hiyo, hebu tuone vile kanuni alizoziweka Mungu kwa ajili ya watu wake wakati huo, zinavyotuhusu na sisi leo. 

Mshikamano wa Upendo (1 Samw.18):