Karibu

Karibu kwenye Tovuti ya CIL. Ligi ya Kutengwa inatoa huduma kwa Kaka na Dada za Christadelphian, na familia zao, ambao wametengwa na eklesia yao. Huduma hutolewa kwa ombi la eklesia yako, hata hivyo unaweza kufikia nyenzo zetu zote kwenye tovuti hii, iwe umejitenga au la.

Huduma zetu ni pamoja na:

  • Mawaidha ya mara kwa mara, Mafunzo ya Biblia na Mihadhara
  • Shule ya Jumapili na Shughuli za Vijana
  • Majarida ya Braille, vitabu na mawasiliano
  • Maktaba ya Rekodi za sauti na video
  • jukwaa la mikutano ya mtandaoni (CIL Meet)

Tafadhali wasiliana nasi ili kujua zaidi.

Ili kupata nyenzo zetu kwenye wavuti yetu, tafadhali jiandikishe na uingie . Unaweza kuona hakikisho hapa chini!

Sasisho za hivi karibuni

Watu watakaookolewa ni wachache?

Jumapili, 21 Septemba 2025
Somo letu la tatu la leo limechukuliwa kutoka katika Luka 13 na 14. Kwenye Luka 13:22 tunakumbushwa kuwa, Yesu alikuwa “Katika safari yake ya kwenda Yerusalemu”. Ni katika majuma yake ya mwisho katika huduma yake, ambapo angeuawa huko. Anavyokwenda anawahubiri waliokuwa tayari kumsikia, akiwa na wanafunzi wake.

Tunachojifunza kwa Hezekia leo

Jumapili, 14 Septemba 2025
Kwenye 2 Wafalme 20 tunasoma juu ya Hezekia akiumwa, na maombi yake kwa Mungu (2 Wafalme 20:1-3). Mungu aliyasikia na kumpa jibu zuri haraka kupitia kwa nabii Isaya (Ms. 4-7).

“Silaha za vita vyetu si za mwili”

Jumapili, 07 Septemba 2025

Masomo: 2 Wafalme 13; Ezekieli 3; 2 Wakorintho 10 - 11 

Kwenye masomo yetu ya leo kuna moja linaloongelewa, juu ya changamoto na matatizo ya mtumishi wa Mungu. Ezekieli alitumwa kuubeba ujumbe wa Mungu kwa mateka waliochukuliwa kutoka Yerusalemu, na anaelezwa kama ni ‘mlinzi’ wao. 

Anakuwa hapendi kwenda lakini analazimika, kwa sababu ya kumtii Mungu. Mungu anampa Ezekieli maono maalumu kwa njia ya makerubi, ili kumhakikishia kuwa yeye yupo wakati wote kazini pamoja na watu wake. Kutekwa na kuwa Babeli hakukuwa ‘mwisho’, ila fursa ya kipekee kama Danieli alivyodhihirisha. 

Ufuateni upendo

Jumapili, 31 Agosti 2025

Masomo: 2 Wafalme 5; Maombolezo 1; Wakorintho 14 

Waraka wa kwanza wa Paulo kwa Wakorintho una mambo ambayo pengine ni magumu na ya kushangaza. Kuna washirika wangapi katika jumuia yetu uliowaona, ambao wanapinga kwa wazi kuwa Yesu alifufuliwa kutoka kwa wafu? 

Ni kama hawapo; lakini hili lilitokea katika karne ya kwanza (1 Wakor. 15:12). Hili lilikuwa mojawapo ya mambo Paulo aliyotaka kuyaweka sawa kwenye nyaraka zake zote mbili. Inaonekana kuna ndugu ambao imani yao ilikuwa imeyumba, na Paulo haonekani kutaka kuwatenga ila kuwasahihisha. 

Sauti Ndogo Ya Utulivu

Jumapili, 24 Agosti 2025

Masomo: 1 Wafalme 19; Yeremia 45-46; 1 Wakorintho 4-5 

Leo hatumsikii Mungu akiongea. Tunao ugumu kujua vile ilivyokuwa, kuisikia sauti ya Mungu au malaika kutoka  mbinguni. Lakini watumishi wengi wa Mungu, na mara nyingine hata maadui zake, walipata kumsikia. Hatujawahi pia kuisikia sauti ya Yesu; tunaweza pengine kuwaonea gere wanafunzi wake waliokuwa naye miaka 2000 iliyopita. 

Lakini, tunayo maneno ya Mungu na ya Mwanawe, yakiwa yamehifadhiwa kwenye kurasa za Biblia. Tunayo kumbukumbu ya maneno aliyoyasema Mungu kwa Adamu na Hawa, kwa Ibrahimu, Musa, Samweli na wengine. 

Kusudi la Moyo

Jumapili, 17 Agosti 2025

Masomo: 1 Wafalme 12; Yeremia 38; Marko 12 

Kusudi la Mungu ni kuijaza dunia watu walio na upendo na ari ya mambo ya KWELI. Upendo na ari hii inatakiwa ionekane kwa namna tunavyoyaishi maisha yetu leo. 

Tunapaswa tuwe taa. Taa haiwashwi na kuwekwa ‘chini ya pishi’; haiwekwi uvunguni au chini ya meza. Taa ni ya kuwaangazia ‘wote waliomo nyumbani’ (Mathayo 5:15). 

Kitabu cha Matendo ya Mitume kina mifano mizuri sana ya wanaume na wanawake wa imani, waliokuwa na ari kubwa ya kuishi maisha yao inavyotakiwa. Waliishi kama ‘dhabihu hai’ mbele ya Mungu wao.